Advertise Here

Friday, October 4, 2013

Mwimbaji Mtanzania Fay Destiny apata Tuzo Marekani.


Mwimbaji wa Nyimbo za injili kutoka Tanzania mwenye asili ya Zanzibar Fay Makame Haji almaarufu kama Fay Destiny ambaye alibadili Dini kutoka Uislamu na kuwa mkristo, ameibuka kidedea katika nafasi ya tatu katika Tuzo za Uimbaji wa Nyimbo za Injili Kimataifa kwa Nchi za Afrika zilizofanyika huko Maryland, Marekani.

Fay amekamata nafasi hiyo baada ya kuchuana vikali na Waimbaji wengine kutoka Mataifa mbalimbali Afrika kama vile Nigeria, Liberia, n.k

Wakati huo huo Fay Destiny anatarajia kuzindua Album yake mpya Jumamosi hii, ambapo Uzinduzi huo utasindikizwa na Waimbaji mbalimbali kama J Sistres na wengine.

Hebu Msikilize hapa akinadi Uzinduzi wake