Advertise Here

Friday, October 25, 2013

Askofu Mwanyika afariki Dunia.

Askofu Mstaafu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Njombe, Raymond Mwanyika amefariki dunia jana mkoani Njombe.

Askofu Mwanyika alizaliwa mwaka 1930 huko kijiji cha Uwemba-Njombe, baada ya makuzi na majiundo yake ya kiroho na kimwili alipata daraja takatifu la Upadre 11/10/1959.

Mnamo 16/01/1971 Baba Mtakatifu Paulo VI alimteua kuwa Askofu wa Njombe, na 25/04/1971 alisimikwa kuwa Askofu rasmi wa Jimbo la Njombe.

June 8 2002 Askofu Mwanyika alipumzika na nafasi yake kuchukuliwa na Askofu Maluma. Askofu Mwanyika amekuwa Padre kwa miaka 54 na Askofu kwa miaka 42.


Atakumbukwa kwa majitoleo yake katika kuwahudumia watu wa Njombe bila kujali tofauti zao za kiimani,alikuwa mstari wa mbele katika kuendeleza huduma za jamii kama hospitali na shule, huduma za maji na umeme katika maeneo mengi ya Njombe, Makete mpaka Ludewa.

Anatarajiwa kuzikwa 29/10/2013 ndani ya Kanisa katoliki la Njombe(Njombe Cathedral).

Bwana alitoa na Bwana ametwaa,jina lake lihimindiwe
Ameeeeeen!

- Jamii Forum -