Advertise Here

Saturday, October 19, 2013

Yaliyojiri kwenye Revival Flames Campus Night ndani ya Saut - Mwanza.

USIKU wa kuamkia leo, ulikuwa ni Usiku wa kusifu na Kuabudu Maarufu kama Revival flames Campus Night iliyoandaliwa na Tafes Saut - Mwanza Campus na kufanyika katika Viwanja vya Shule ya Msingi Nyamalango kuanzia Mida kama ya Saa 3:00 Usiku na Kumalizika Mida kama ya Saa 10 usiku.

Vikundi mbalimbali vya Kusifu na Kuabudu vilihudumu katika Mkesha huo kama Vile Tafes Saut Praise & Worship Team, Tafes Choir, Huima Choir, n.k huku Neno la Mungu likitolewa na Pastor elisha Msanifu kutoka Kanisa la Highway of Holiness Cathedral lililopo Ilemela Jijini Mwanza.

Mbali ya vikundi hivyo kutoka chuo cha SAUT Mwanza, pia kundi Maarufu Maarufu la Glorious Worship Team(GWT) kutoka dar es salaam pia lilipata fursa ya Kuongoza sifa katika Usiku huo.

Sasa Tazama namna mambo yalivyokuwa Viwanjani hapo
Watumishi wa Mungu wakiwa Viwanjani hapo
Tafes Praise Team On Stage




Sasa mida kama ya Saa 7 hivi wakaingia glorious Worship Team na Mambo yakawa hiviiii...
Kwenye Mic ni Paul Clement



Emma Solo wa GWT

Sifa na Utukufu zirudi kwake yeye aliye Mkuu kupita wote Mbinguni na Duniani.

- Picha zote na Elia Migongo -