Advertise Here

Monday, November 18, 2013

Andrew Palau akamilisha Mkutano wa "Love Ethiopia Festival" Nchini Ethiopia.

Andrew Palau(Wa pili kushoto kwa walioketi) akiwa na Wachungaji mbalimbali wa Nchini Ethiopia
Mwinjilisti wa Kimataifa Andrew Palau, amemaliza Mkutano mkubwa wa Injili Nchini Ethiopia, Mkutano uliopewa Jina la "Love Ethiopia Festival". Mkutano huo umefanyika Novemba 16 na 17, 2013.

Katika Mkutano huo, Waimbaji mbalimbali wa ndani na Nje ya Ethiopia walihudumu, akiwepo Mwimbaji wa Kimataifa Don Moen. Mkutano huo mkubwa ulifanyika Mji Mkuu wa Ethiopia, Addis Ababa.

Mkutano huo pia ulihusisha utoaji wa Huduma mbalimbali za Kijamii, kama vile matibabu ya Macho. Pia michezo mbalimbali kama vile Kuendesha baiskeli ukitokea kuwavuta watu mbalimbali waliofika kwenye Mkutano huo.

Tazama Picha hizi uone Mambo yalivyokuwa huko Ethiopia
Watu wakipata Matibabu
Mwendesha Baiskeli akisalimia Mashabiki zake
Kazi ikiendelea
Andrew Palau akihubiri
Injli ikiendelea
Mamia ya watu wakiwa kwenye Mkutano
Haleluyah!!!
Mass Choir ya Ethiopia ikihudumu
Don Moen akihudumu kwenye Mkutano huo
Eneo la Tukio
Watu wakifuatilia kwa Makini kinachoendelea Madhabahuni
Wakati wa Maombi
Mkutano kama huu, uliwahi kufanyika Tanzania ukipewa Jina la "Love Tanzania Festival" ambapo Waimbaji kama Don Moen na Nicole C. Mullen walihudumu katika Mkutano huo, uliofanyika Viwanja vya Jangwani August 11 na 12, 2012.