Advertise Here

Tuesday, November 19, 2013

Mtoto wa Kiroho wa TB Joshua alitabiri Matokeo ya Nigeria na Ethiopia.

TB-Joshua-and-Onazi
Mtoto wa kiroho wa Tb Joshua ambaye pia ni Mchezaji wa Timu ya Taifa ya Nchini Nigeria(Super Eagles), Midfilder Ogenyi Onazi alitabiri Matokeo kati ya Timu yao ya Nigeria na Ethiopia uliochezwa Novemba 16, na Matokeo kuwa 2-0 kwa Nigeria kushinda bao 2.

Siku ya Ijumaa Novemba 15, Mchezaji huyo ambaye ni Mshirika wa Kanisa la SCOAN la Nchini Nigeria lililochini ya TB Joshua, alitabiri kuwa Nigeria itashinda 2-0 katika Mchezo huo, na ndivyo ilivyokuwa.

Utabiri wa mchezaji huyo umewashtua watu wengi kwa kuweza kuotea kwa Usahihi jambo lililowafanya watu kuhisi kuwa Utabiri huo ulitolewa na TB Joshua.

Jambo hili limefanya Mchezaji huyo wa Nigeria Onazi kupewa jina la Nabii mtoto. Ushindi huo uliwapa nafasi Timu ya Nigeria(Super Eagles) kufuzu Tiketi ya Kushiriki Mashindano ya Kombe la Dunia.