Advertise Here

Wednesday, November 20, 2013

Cheka na Mc Pilipili - Episode 1.

Leo tunaanza Kipengele kipya kabisa ambacho kitakuwa kinakujia kila Siku ya Jumanne. Segment hii itaitwa, "Cheka na Mc Pilipili".

Mc Pilipili ni Mc maarufu sana Tanzania, na pia ni Mchekeshaji aliyejivunia umaarufu Mkubwa sana ndani na nje ya Tanzania. Kabila lake ni Mgogo wa Dodoma. Ni Mc aliyepitia mambo mengi sana katika Maisha yake, hasa Ugumu wa maisha aliokumbana nao wakati anaanza shughuli hizi. Tutaweka Historia ya Mc Pilipili siku chache zijazo.

Mc Pilipili a.k.a Handsome wa Kigogo, pia aliwahi kuwa Mwalimu wa Shule za Sekondari kwa Miaka 7 huko Dodoma, Tanzania na baadaye kuacha kazi hiyo kisha kuwa Mchekeshaji na Mc kwenye Shughuli mbalimbali.

Sasa leo katika "Cheka na Mc Pilipili", tunaanza na Kichekesho hiki Kuhusu mambo ya "Cinema". Sasa Cinema kuna mambo gani??? Tazama Video hii hapa

Wasiliana na Mc Pilipili
0715 415542
0754 415542