Advertise Here

Tuesday, November 19, 2013

Mwimbaji Mr. Boo wa Kenya kufanyiwa Upasuaji.

Mr. Boo
Mwimbaji wa Nyimbo za Injili toka Nchini Kenya maarufu kama Mr. Boo, anatarajiwa kufanyiwa upasuaji mwingine. Upasuaji huu unafuatia Upasuaji mwingine aliofanyiwa Mr. Boo wa kutoa vipande vya Mawe katika Figo yake.

Mwimbaji huu alimpoteza Mama yake mzazi mwaka huu, na wiki chache baada ya Kifo cha Mama yake alifanyiwa Upasuaji.

Mr. Boo anasema Upasuaji huu unaofanyika mara kwa mara umekuwa ukimuathiri sana kimwili na kifedha kwa huwa inatumia pesa nyingi sana kwa ajili ya zoezi kama hilo.

Kumbuka kumuweka Mwimbaji huyu katika Maombi ili Mungu amuepushe na Matatizo haya ambayo yamekuwa yakimsumbua Mara kwa Mara.

Huu ni Wimbo wa Mr. Boo ujulikanao kama "Sugua", Wimbo aliomshirikisha Mwimbaji Angel