Advertise Here

Saturday, November 2, 2013

Mke wa Makamu wa Rais wa Kenya aenda Zimbabwe kwa Maombi.

Mrs Ruto said the charges against Mr Ruto came as a shock to the family.
Rachel Ruto, Mke wa Makamu wa Rais wa Kenya William Ruto
Rachel Ruto ambaye ni Mke wa Makamu wa Rais wa Kenya William Ruto yupo Zimbabwe kwa Kikao cha Maombi na Mtume wa Spirit Embassy(Zimbabwe) Mtume Ubert Angels.

Mrs. Ruto ambaye ni rafiki wa Karibu wa Mke wa Mtume Ubert Angels, Beverly Angels amewasili Zimbabwe jana Mchana na ni Mgeni Rasmi katika Kongamano la Mwaka la wanawake lililoandaliwa na Spirit Embassy.

Kongamano hilo lililoanza jana jioni katika Jengo la "Spirit Embassy Royal Towers" katika Mji wa Harare, limekusanya zaidi ya Wageni wa Kimataifa 500.

Moja ya wageni muhimu katika Kongamano hilo ni Pastor Dona Ndifoni kutoka Marekani, na Kongamano hilo linadumu kwa Siku Mbili.