Advertise Here

Thursday, November 21, 2013

Mwinjilisti wa Kimataifa Billy Graham alazwa hospitali kwa Matatizo ya Upumuaji.

Billy Graham
Billy Graham, siku ya birthday yake ya Kutimiza Miaka 95
Mwinjilisti wa kimataifa Billy Graham amelazwa katika Hospitali ya Asheville Jumanne ya Wiki hii baada ya kukumbwa na Matatizo katika Mfumo wake wa Upumuaji.

Graham ambaye ametimiza Miaka 95 Mwanzoni mwa Mwezi huu, anatarajiwa kuruhusiwa kurudi nyumbani siku yoyote kuanzia leo.

"Bw. Graham yuko hospitali akisumbuliwa na Matatizo ya Upumuaji, tatizo alilokuwa nalo pia wiki chache zilizopita. Hivyo tunatarajia ataruhusiwa wakati wowote ndani ya siku hizi mbili". Alisema Msemaji wa Graham.

Graham ambaye hakuwahi kuhubiri kwenye Umati wa watu kwa takribani Miaka 7, Sauti yake ilisikika tena katika birthday yake, akihubiri huku akiwa amerekodiwa.