Advertise Here

Monday, November 25, 2013

Kwa mara ya kwanza Papa Francis aonesha Mabaki ya Mtakatifu Petro.

Waumini wa Kanisa Katoliki duniani wameoneshwa kwa mara ya kwanza mabaki  ya Mtakatifu Petro toka kupatikana kwake Miaka ya 1940.

Mabaki hayo ya Mtakatifu Petro, yalioneshwa kwa waumini hao huku yakiwa yamewekwa katika kisanduku katika misa  iliyo ongozwa na Papa Fransisco jumapili ya Jana.


Kuoneshwa kwa mabaki hayo kwa waumini wa kanisa Katoliki inaaminika kutaongeza Imani ya waumini wa kanisa hilo, hasa baada ya kukumbwa na  mikasa ya utovu wa nidhamu ya kimaadili kwa wafanyakazi na wahudumu wa kanisa hilo katika sehemu tofauti duniani.

Tazama Video hii ya Papa Francisco akionesha Mabaki hayo

- Kwa Msaada wa Launite Blog -