Advertise Here

Tuesday, November 26, 2013

Hawa ndio Wachungaji Watano Matajiri Nchini Nigeria.

Bishop David Oyedepo
1. Bishop David Oyedepo
Ni mwanzilishi wa Huduma ya "Living Faith World Outreach Ministry" maarufu kama Winners Chapel. Anaamika kuwa na Utajiri wa Dolla za Kimarekani 150. Alianzisha kanisani hilo Mwaka 1981, na kuanzia hapo likaanza kukua na kuwa Kanisa lenye waumini wengi sana Nchini Nigeria.

Bishop Oyedepo anamiliki ndege 4 binafsi na ana Makazi London na Marekani. Ni mwandishi wa Vitabu na pia anamiliki Kampuni ya Uchapishaji ijulikanayo kama Dominion Publishing. Mbali ya hayo, pia ana miliki Chuo Kikuu kijulikanacho kama Covenant University, Shule ya Faith Academy na Elite High School.


Richest Pastors
2. Chris Oyakhilome
Ni mwanzilishi wa Huduma ya "Believers' Loveworld Ministries" maarufu kama Christ Embassy. Ana utajiri kati ya Dolla za kimarekani Millioni 30 - Millioni 50. Kanisa lake lina Washirika zaidi ya Elfu Arobaini(40,000).

Anamiliki Kituo cha Luninga, Magazeti, Majarida, Hotel, na mengineyo. Kanisa lake lina Matawi Nigeria, Afrika Kusini, London, Canada, na Marekani. Kituo chake ca Luninga ndiyo kinachoamika kuwa kituo cha Kwanza cha Kikristo kurusha Matangazo yake Afrika Nzima kwa Masaa 24.

nigeria
3. Temitope Balogun Joshua (TB Joshua)
Ni mwanzilishi wa Kanisa la "Synagogue Church of All Nations (SCOAN)". Inaaminika kuwa ana utajiri wa dolla za Kimarekani kati ya Millioni 10 - Millioni 15. Alianzisha Kanisa hilo Mwaka 1987, na kwasasa ana Waumini zaidi ya Elfu Kumi na Tano(15,000).

Kanisa lake lina Matawi ghana, UK, Afrika Kusini na Ugiriki. Kwa miaka kadhaa iliyopita, TB Joshua ameweza kuchangia huduma mbalimbali kama vile Elimu, Afya na Huduma za Matengenezo mbalimbali kwa zaidi ya Dolla za kimarekani Millioni 20. Ana miliki pia Kituo cha Luninga cha Emmanuel Tv.


Matthew Ashimolowo Net Worth
4. Matthew Ashimolowo
Ni mwanzilishi wa Kanisa la "Kingsway International Christian Centre (KICC)". Anatajwa kuwa na Utajiri wa Dolla za Kimarekani kati la Millioni 6 - Millioni 10. Mwaka 1992 alitumwa na Kanisa lake la awali la "Foursquare Gospel Church" la Nchini Nigeria kwenda kufungua tawi London, na badala yake akafungua Kanisa lake la "Kingsway International Christian Centre (KICC)" ambalo ni Moja ya Kanisa Kubwa sana huko UK.

Mshahara wake kwa Mwaka Mmoja ni Dolla za Kimarekani Laki 2(200,000) na Kiasi cha Utajiri wake mwingine kinatoka kwenye biashara anazofanya ikiwa ni pamoja na kampuni yake inayoandaa Makala mbalimbali za kikristo.


Chris Okotie Net Worth
5. Chris Okotie
Ni mwanzilishi wa Kanisa la "Household of God Church". Okotie alikuwa Mwanamuziki wa Pop miaka iliyopita na baadaye aliamua kuokoka na kuwa Muhubiri baada ya Miaka kadhaa.

Kanisa lake linakadiriwa kuwa na Waumini Elfu Tano(5,000) ambao wengi wao ni Watu maarufu wa Nigeria kama wanamuziki. Amegombea Urais wa Nigeria mara tatu na hakufanikiwa kushinda hata mara moja.

Orodha hii ni kwa Mujibu wa Mtandao wa "Celebrity Networth" iliyotolewa Mwezi wa 8, Mwaka huu.