Advertise Here

Sunday, November 24, 2013

Kulola Junior na Frolian Katunzi watikisa Jiji la Mwanza.

Mkutano wa Injili ulioandaliwa na Kanisa la EAGT City Centre chini ya Mchungaji Michael G. Kulola(Kulola Junior) umeanza katika Viwanja vya Furahisha jijini Mwanza na utadumu kwa Siku 8.
Wanenaji katika mkutano huo ni Mchungaji Frolian Katunzi kutoka Dar es salaam, Mchungaji Frank Msuya toka Arusha na Mchungaji Michael Kulola toka Mwanza.
Kwaya mbalimbali pamoja na Waimbaji mbalimbali wanahudumu katika Mkutano huo kama vile Bugando Injili, City Centre Choir, Mlima wa Utukufu(Ilemela), Lusekelo kutoka Dar, na wengineo.