Advertise Here

Saturday, November 23, 2013

Wimbo wa "Nitumezi" wa Bumie toka Zambia wafanya vizuri kwasasa.

Mwimbaji wa kike anayefanya vizuri Nchini Zambia Born Bunmi Dada a.k.a Bumie, Wimbo wake wa "Nitumezi" ukiwa na maana ya "Asante" unafanya vizuri sana kwasasa.

Bumie mwenye asili ya Lagos-Nigeria baada ya kukamilisha wimbo wa "Nitumezi", Wimbo huo umepata nafasi ya Kuchezwa sana kwenye Radio mbalimbali huko Zambia.

Album ya kwanza ya Bumie ilijulikana kama "My All" na ilitoka mwanzoni mwa huu. Kupitia Album hiyo, Bumie ameweza kupata mialiko mbalimbali ndani na nje ya Nchi ya Zambia, kama Marekani ambako alionekana kwenye Vipindi mbalimbali vya Runinga na Kusikika kwenye Radio.

Bumie anayesifika sana pia kwa Uzuri wake, pia ana sauti nzuri ambayo ameamua kuitumia katika Kumsifu Mungu.