Advertise Here

Thursday, November 28, 2013

Waimbaji maarufu Nigeria wafunga ndoa.

Grace akiwa na Emmanuel
Waimbaji Maarufu wa Nyimbo za Injili nchini Nigeria Grace Okoduwa (Jahdiel) and  Emmanuel Benjamin (Eben) ambao wote ni washirika wa Kanisa la Christ Embassy, wamefunga ndoa ya asili Novemba 23 Mwaka huu, huku wakitarajia kufunga ndoa ya Kikristo Jumamosi hii ya Novemba 30 Mwaka huu.

Ndoa hiyo itafungwa katika Kanisa la Christ Embassy, na Itafungwa na Pastor Chris Oyakhilome, Mwanzilishi wa Kanisa hilo Ulimwenguni.

Grace Okoduwa (Jahdiel) anajulikana zaidi kwa wimbo wake maarufu ujulikanao kama "Heritage" na Emmanuel Benjamin (Eben) akijulikana zaidi kwa wimbo wa "Imaramma".

Hizi ni Picha za harusi yao ya Kiasili
Grace na Emmanuel
 
 
 
 
Tazama wimbo wa Jahdiel(Grace) Ujulikanao kama "Heritage"