Advertise Here

Saturday, November 16, 2013

Makanisa Nchini Zimbabwe yakataa kulipa Kodi.

Wakati serikali ya Zimbabwe ikifikiria kuyatoza kodi Makanisa Nchini Zimbabwe, Viongozi mbalimbali wa Makanisa Nchini humo, wamepinga hatua hiyo huku wakisema Makanisa hayapaswi kulipa kodi mana yanafanya kazi ambayo Serikali imeshindwa kuifanya hivyo kwao ni kama Unyanyasaji kwa Makanisa.

Wakati hayo yakiendelea, Mkuu wa Mawasiliano wa Mamlaka ya Mapato Zimbabwe, Taungana Ndoro amesema hana kauli rasmi kuhusiana na Ukandamizaji huo kwa Makanisa kwani kuna timu maalumu iliyoundwa kuchunguza swala hilo hasa vyanzo vya Mapato ya Makanisa.

Askofu Noah Pashapa wa Kanisa la "Life and Liberty" amesema Makanisa hayapaswi kuliko Kodi, isipokuwa kwa yale Makanisa yanayoendeshwa kama Biashara, hayo ndo yalipe Kodi.

Hapa Askofu Pashapa anasema, "Kuna Makanisa yanaendeshwa kama Biashara kwa kua yanamilikiwa na watu na wananufaika na Sadaka pamoja na Mafungu ya Kumi moja kwa moja. Na pia kuna Makanisa yanayoendeshwa Kiimani zaidi na hayategemei faida, huku kipato kikielekezwa katika Maendeleo ya Kijamii".

Aliongeza kuwa, Makanisa hayo yanayojiendesha kibiashara, ndiyo yanayopaswa kulipa Kodi.