Advertise Here

Friday, November 15, 2013

Sonnie Badu asherehekea Birthday yake na Watoto yatima huko Ghana.

Sonnie Badu orphans
Sonnie Badu akiwa na watoto yatima
Mwimbaji wa Kimataifa wa Nyimbo za injili aliyegusa Maisha ya watu mbalimbali kwa nyimbo zake, Sonnie Badu Jumamosi iliyopita yaani Novemba 9, alisherehekea siku yake ya kuzaliwa na Watoto yatima katika Vituo vinne tofauti huko Ghana.

Alitembelea Vituo vya Remar Ghana Christian Rehabilitation Center in Dansoman, Teshie Orphanage, New Life Orphanage International kilichopo Nungua na Lighthouse Christian Children’s Home kilichopo Aburi.

Katika vituo vyote alivyotembelea, watoto waliandaliwa kwa ajili ya kumlaki Sonnie kwa Nyimbo maarufu kama "Baaba" na "Let it rain".

Katika kila eneo alilotembelea, alikula pamoja na watoto hao keki yake ya birthday pamoja na kuchangisha kiasi cha pesa kwa ajili ya kuwasaidia watoto hao.

Sonnie aliwasili Ghana wiki iliyopita kwa ajili ya Maandalizi ya Tamasha atakalolifanya Nchini Ghana Novemba 30, Mwaka huu.