Advertise Here

Monday, November 25, 2013

Yaliyojiri kwenye "Nataka Nimjue" ya Christina Shusho.

Christina Shusho
Kwa Mara ya Kwanza katika Historia ya Muziki wa Christina Shusho toka Tanzania, Jana ilikuwa ni Siku ya Live DVD Recording yake iliyofanyika pale City Christian Centre, Upanga Jijini Dar es salaam.

Watu wengi wamezoea kumuona Christina Shusho akiimba kwa Kutumia CD "Playback", lakini Jana aliudhihirishia Uma kuwa hata kuimba LIVE pia anaweza. Kazi hiyo kubwa imefanywa chini ya Music Director Samuel Yonah.

Katika tukio hilo, waimbaji mbalimbali walikuwepo kumsindikiza Christina Shusho kama vile Upendo Kilahiro, The Voice Acapella, na wengineo

Mambo yalikuwa hivi
Shusho On Stage
Backups wakienda sawa
Ilikuwa ni Shangwe na ndelemo
Hii ilikuwa ni Collabo kati ya Shusho na The Voice
Kila chombo kilikuwepo kuhakikisha Mungu anapewa Utukufu wa kutosha
Hiki ndo Kikosi kazi

- Picha zote na Uncle Jimmy -